Sunday, June 21, 2015

ADHABU YA NEYMAR ITAKAVYO MGHARIMU

Neymar-kadi
Hii sio taarifa nzuri kwa fans wa Brazil baada ya staa wao Neymar kupunguzwa kenye Kikosi cha Timu hiyo.
Neymar amefungiwa mechi nne  kutokana na utovu wa nidhamu Uwanjani ambapo alichukua mpira na kumpiga nao mgongoni Mchezaji wa Colombia, Pablo Armero ambapo katika mechi hiyo Brazil walifungwa 1-0.
Neymar alioneshwa kadi nyekundu na hukumu ya kwanza iliyotolewa ilikuwa Neymar akose mechi moja tu, lakini baadae Shirikisho la Soka Amerika Kusini walipitia upya kesi yake na kumwongezea adhabu na kumfungia mechi nne baada ya kugundua alitoa kauli mbaya kwa mwamuzi Enrique Osses.
Neymar-Copa-1
Staa wa Colombia, Carlos Bacca nae kafungiwa kucheza mechi mbili lakini Shirikisho hilo limesema milango iko wazi kama jamaa wakiamua kukata rufaa

0 comments:

Post a Comment

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More