Uzazi
wa mpango ni jambo ambalo husisitizwa ndani ya jamii ili kuwa na
familia bora na uwezo wa kutunza familia kutokana na idadi ya watoto
wanaozaliwa.
Mike Holpin hakuona
umuhimu wala hana habari na uzazi wa mpango kwani licha ya kuwa na
watoto 40 bado anafikiria kuongeza wengine huku akiamini hata vitabu vya
dini vinaruhusu.
Mwanaume huyo mwenye miaka 56 mwenyeji wa Monmuothshire, Uingereza
alipata mtoto wake wa kwanza akiwa na miaka 19 tu na kwa sasa mtoto
wake wa kwanza ana miaka 37 huku wa mwisho akiwa na miaka mitatu.
Watoto
hao amezaa na wanawake 20 tofauti na amesisitizi yupo tayari kuongeza
wengine kwani hata vitabu vya dini vimeruhusu na ameamua kujichora
tattoo yenye majina ya watoto wake ili aweze kuwakumbuka.
Aliongeza kati ya wanawake 20
aliowazalisha sita ndio aliweza kuishi nao lakini baadae alitengana nao
kutokana na tabia yake ya kutokuwa mwaminifu pamoja na kuwanyanyasa.
0 comments:
Post a Comment