Friday, November 25, 2016

Tuhuma zinazoweza kumpeleka Eto’o miaka 10 jela

Moja kati ya habari zinazogonga vichwa vya habari barani Ulaya leo November 24 ni kuhusiana staa wa kimataifa wa Cameroon anayeichezea Antalyaspor ya UturukiSamuel Eto’o kuandikwa kuwa anaweza kukumbana na kifungo cha miaka 10 jela pamoja na faini.
Stori kutoka 101greatgoals.com imeandika kuwa staa huyo wa Cameroon anaweza kufungwa miaka 10 jela na faini ya euro milioni 14 ambazo ni zaidi ya Tsh bilioni 30 kwa kosa la ukwepaji kodi akiwa Hispania katika kipindi kati ya mwaka 2006 na 2009 kupitia mauzo ya haki ya picha zake.
Eto’o alicheza na kuishi Hispania akiwa anaichezea FC Barcelona kuanzia mwaka 2004 hadi mwaka 2009 alipoamua kuhama na kujiunga na Inter Milan ya Italia na baadae kwenda kucheza soka Urusi katika klabu ya Anzhi Makhachkala

0 comments:

Post a Comment

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More