Sunday, March 20, 2016

MIMI PEKEE NDIYE MWENYE UBAVU WA KUPAMBANA NA DIAMOND CHA MSINGI NI MASLAHI TU HARAFU TUKUTANE PALE UWANJA WA TAIFA SHAMBA LA BIBI

Juma Nature asema yeye ndiye mwenye ubavu wa kupambana na Diamond Platnumz na wala si Ali Kiba,Kupitia Fnl Juma Nature aliniambia kuwa anaomba mpambano huo ufanyike kwenye Uwanja wa Taifa wa zamani [Shamba la bibi].

“Diamond ndiye anakalia game ya muziki nchini kwa sasa, na muziki ni furaha basi nataka kupambana naye kwenye uwanja wa Taifa na mashabiki wakitazama huku kusema nani ni mshindi, Diamond ndiye kaiteka game kuliko Alikiba na kama viongozi wapo tayari kuunga mkono na kutengeneza muziki mzuri basi waandae tamasha hilo”

Pia Nature amezungumzia kuhusu kufanya kazi na Said Fela ambapo majuma kadhaa yaliyo pita Fela alizungumzia kuhusu kufanya kazi na Juma Nature nakusema kama ikitokea ataweza kufanya naye kazi.

”Mimi sina tatizo lakini maslahi kwanza, kama kufanya naye kazi itabidi tuandikishane mkataba kwanza”.

0 comments:

Post a Comment

Share

Twitter Delicious Facebook Digg Stumbleupon Favorites More